News

RASMI…SIMBA KUFYEKA WATANO DIRISHA DOGO…WAWA, BOCCO NA NYONI WATAJWA…BARBARA AFUNGUKA..

admin December 15, 2021 5:25 am


SIMBA huenda ikaachana na wachezaji watano mwishoni mwa msimu huu mara baada ya mikataba yao kumalizika, kati ya hao yupo beki Muivory Coast, Pascal Serge Wawa.

Hiyo ni katika kuhakikisha wanakuwa na kikosi imara kitakachofanya vizuri msimu ujao kwenye mashindano mbalimbali. Tayari uongozi wa Simba umeanza kufanya mazungumzo na baadhi ya wachezaji wapyawatakaowasajili.

Mmoja wa mabosi wa Simba, ameliambia amesema kuwa,  wachezaji hao baadhi wataachwa kutokana na umri mkubwa walionao.

Bosi huyo alisema wachezaji hao wamekosa kasi, hivyo Kocha Mkuu, Pablo Franco amependekeza wachezaji hao ambao majina yao yamefichwa kwa sasa.

Aliongeza kuwa, tayari majina hayo kocha ameyakabidhi kwa uongozi, hivyo mwishoni mwa msimu watatangazwa.

“Zaidi ya wachezaji watano huenda Simba wakaachana nao mwishoni mwa msimu, kati ya hao yupo Wawa.

“Kwa sasa hapati nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza, nafasi yake imechukuliwa na Inonga (Hennock) ambaye anacheza kwa kuelewana na Onyango (Joash).

“Wachezaji wengine wanaotajwa ni wale ambao umri umekwenda na hawapati nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza,” alisema bosi huyo.

Miongoni mwa wachezaji wenye umri mkubwa ni pamoja na John Bocco, Erasto Nyoni, Meddie Kagere na Mzamiru Yassin

Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez, hivi karibuni alizungumzia usajili kwa kusema: “Tumepanga kufanya maamuzi magumu katika usajili wetu kwa kusajili wachezaji wenye uwezo mkubwa watakaofanya vema katika mashindano ya kimataifa.”

KISA CHAMA..YANGA NA SIMBA WAMEANZA UPYAA…SIMBA WAVAMIA TFF..WATUA NA FAILI ZITO.. BAADA YA KUONA WENZAKE WALIVYOCHEZA DHIDI YA SIMBA…YACOUBA AIBUKA NA HILI ..ATUPA DONGO…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply