Home news KUELEKEA MICHAUNO YA CAF…PABLO ASHANGAZA UMAA..HAJUI LOLOTE…AMTAJA CHAMA TENA…

KUELEKEA MICHAUNO YA CAF…PABLO ASHANGAZA UMAA..HAJUI LOLOTE…AMTAJA CHAMA TENA…


KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco, ameichungulia droo ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika na kufunguka kuwa, wanatarajia kukutana na upinzani mkubwa katika hatua hiyo huku akimtaja Clatous Chama kama miongoni mwa mastaa hatari ambao inabidi wajipange kuwadhibiti.

Jumanne wiki hii droo ya hatua ya makundi ya Kombe la ShirikishoAfrika ilipangwa kwenye makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf), Cairo jijini Misri ambapo Simba wameangukia Kundi D pamoja na timu za RS Berkane ya Morocco, USGN ya Niger na ASEC Mimosas ya Ivory Coast.

Katika hatua hiyo, Simba wanatarajia kuanza kibarua chao cha kwanza nyumbani kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam ambapo wataikaribisha ASEC Mimosas kutokea Ivory Coast Februari 13, mwaka 2022.

Akizungumza na Gazeti la  Championi , kocha Pablo alisema: β€œKwanza napenda kuweka wazi kuwa siwajui sana wapinzani tuliopangwa nao kwenye Kundi D la Kombe la Shirikisho Afrika, lakini najua kuwa tunakwenda kucheza dhidi ya timu ngumu kwani baadhi zimekuwa na rekodi nzuri kwenye soka laAfrika.

β€œLakini pia tutacheza dhidi ya timu kama RS Berkane ya Morocco ambayo ni miongoni mwa timu zenye wachezaji bora, najua hata Clatous Chama ni miongoni mwa wachezaji wanaocheza kwao na ni hatari, hivyo tunatarajia upinzani mkubwa lakini tunajiamini na tuna matumaini makubwa ya kufuzu.”

SOMA NA HII  KISA USHINDI WA 7-0...MBRAZILI SIMBA AITAKA MAMELOD SUNDOWN ROBO FAINAL...