Home news KUELEKEA MECHI YA CAF…HAWA HAPA MASTAA MUHIMU WA SIMBA WATAKAOKOSEKANIKA…

KUELEKEA MECHI YA CAF…HAWA HAPA MASTAA MUHIMU WA SIMBA WATAKAOKOSEKANIKA…

 


Kocha wa Kikosi cha Simba, Pablo Franco Martín amesema kuwa Katika mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho Afrika (CAF) dhidi ya ASEC Mimosas 🇨🇮 watawakosa nyota wao watano kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo majeruhi.

Wachezaji hao ni mshambuliaji Chris Mugalu 🇨🇩 ambaye amevunjika mkono hivyo hatahusika katika mchezo huo, Kibu Denis 🇹🇿 ambaye anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi leo, Clatous Chama 🇿🇲 Hatashiriki kabisa michuano hiyo kutokana na kanuni za (CAF), Thadeo Lwanga majeruhi na Bernard Morrison 🇬🇭 aliye simamishwa kutokana na utovu wa nidhamu.

Simba, Februari 13, 2022 saa 10:00 jioni watashuka Katika dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam kumenyana na ASEC Mimosas ya Ivory Coast 🇨🇮 katika mchezo wa Kombe la Shirikisho AFRIKA.

SOMA NA HII  KUHUSU CHAMA KURUDI TENA TZ...NI SUALA LA MUDA TU...AFUNGUKA KILA KITU..AGUSIA MKWANJA WA YANGA...