Home news KUELEKEA MECHI YA CAF…HAWA HAPA MASTAA MUHIMU WA SIMBA WATAKAOKOSEKANIKA…

KUELEKEA MECHI YA CAF…HAWA HAPA MASTAA MUHIMU WA SIMBA WATAKAOKOSEKANIKA…

 


Kocha wa Kikosi cha Simba, Pablo Franco Martรญn amesema kuwa Katika mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho Afrika (CAF) dhidi ya ASEC Mimosas ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ watawakosa nyota wao watano kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo majeruhi.

Wachezaji hao ni mshambuliaji Chris Mugalu ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ ambaye amevunjika mkono hivyo hatahusika katika mchezo huo, Kibu Denis ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ ambaye anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi leo, Clatous Chama ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฒ Hatashiriki kabisa michuano hiyo kutokana na kanuni za (CAF), Thadeo Lwanga majeruhi na Bernard Morrison ๐Ÿ‡ฌ๐Ÿ‡ญ aliye simamishwa kutokana na utovu wa nidhamu.

Simba, Februari 13, 2022 saa 10:00 jioni watashuka Katika dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam kumenyana na ASEC Mimosas ya Ivory Coast ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ katika mchezo wa Kombe la Shirikisho AFRIKA.

SOMA NA HII  KAGERA SUGAR: SIMBA NI TIMU KUBWA,USIPOKUWA NA MBINU UTAFUNGWA MABAO MENGI