Kocha wa Kikosi cha Simba, Pablo Franco Martรญn amesema kuwa Katika mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho Afrika (CAF) dhidi ya ASEC Mimosas ๐จ๐ฎ watawakosa nyota wao watano kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo majeruhi.
Wachezaji hao ni mshambuliaji Chris Mugalu ๐จ๐ฉ ambaye amevunjika mkono hivyo hatahusika katika mchezo huo, Kibu Denis ๐น๐ฟ ambaye anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi leo, Clatous Chama ๐ฟ๐ฒ Hatashiriki kabisa michuano hiyo kutokana na kanuni za (CAF), Thadeo Lwanga majeruhi na Bernard Morrison ๐ฌ๐ญ aliye simamishwa kutokana na utovu wa nidhamu.
Simba, Februari 13, 2022 saa 10:00 jioni watashuka Katika dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam kumenyana na ASEC Mimosas ya Ivory Coast ๐จ๐ฎ katika mchezo wa Kombe la Shirikisho AFRIKA.