Home news WABABE WA SIMBA WATUA YANGA…WATOA KAULI YA KIBABE MNOOO…

WABABE WA SIMBA WATUA YANGA…WATOA KAULI YA KIBABE MNOOO…


HADI sasa ni Yanga pekee ambayo haijapoteza mchezo wowote kwenye Ligi Kuu Bara lakini unaambiwa Mbeya City wanataka kuweka rekodi na historia ya kuwazima vigogo wote wa soka nchini kuhakikisha vinara hao nao wanakaa.

Mbeya City licha ya kutovuma, lakini imekuwa ya moto msimu huu baada ya kutembeza vipigo ikiwamo dhidi ya bingwa mtetezi, Simba na Februari 5 watawavaa Yanga kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Nahodha wa timu hiyo, Paul Nonga alisema wao msimu huu kila mechi ni vita ya pointi tatu na hawaangalii wanacheza na nani kwani wanafahamu timu yoyote ya Ligi Kuu ni ngumu.

“Sisi kila mechi tunataka pointi tatu na msimu huu tumeweka malengo, tunashirikiana wachezaji wote kuhakikisha tunapata ushindi, Yanga tunawaheshimu ila hatuwaogopi,” alisema Nonga.

Naye kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ alisema wanafahamu mchezo utakuwa mgumu kutokana na rekodi waliyonayo wapinzani, lakini Mbeya City hawana presha na matarajio ni ushindi.

“Mchezo utakuwa mgumu na ushindani, kila mmoja anataka ushindi, tunajua Yanga ni timu kubwa na wachezaji wake, lakini hatuna hofu binafsi nimejipanga kuendeleza rekodi ya kutofungwa,” alisema Dida.

Kocha mkuu wa timu hiyo, Mathias Lule, alisema Yanga ni kama timu nyingine na mchezo huo ni wa kawaida kama zilivyopita nyingine na kwamba vijana wake wako fiti.

“Hii ni ligi hakuna cha Yanga au nani, kimsingi vijana wangu wako fiti kisaikolojia na kiufundi.” na wako tayari kwa mchezo huo tukiamini tutashinda,” alisema Lule.

SOMA NA HII  AFCON 2023:- MUISRAEL WA ZAMBIA APANIA KUIFANYA KITU MBAYA TANZANIA...