Home Habari za michezo KUELEKEA MECHI NA NAMUNGO….MANARA KAONA ISIWE TABU..KAAMUA KUIBUKA NA HILI JIPYA….

KUELEKEA MECHI NA NAMUNGO….MANARA KAONA ISIWE TABU..KAAMUA KUIBUKA NA HILI JIPYA….


Afisa Habari wa Yanga, Haji Manara amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mechi zote watakazocheza na kikubwa wanahitaji pointi tatu ambazo kwao ni muhimu .

Kikosi cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi kinatarajiwa kushuka uwanjani Aprili 23 kusaka pointi tatu dhidi ya Namungo FC katika uwanja Benjamin Mkapa.

β€œTunaua mchezo wetu dhidi Namungo utakuwa na ushindani mkubwa, wapinzani wetu tunawaheshimu hivyo ambacho tunakifanya ni maandalizi mazuri”

”Wachezaji wapo tayari na kila kitu kinakwenda sawa hivyo mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi ili kuweza kuona namna gani tunapata matokeo,” amesema Haji Manara.

Ni mchezo wa ligi ambapo utakuwa ni wa mzunguko wa pili baada ya ule wa awali walipokutana Uwanja wa Ilulu ubao kusoma Namungo 1-1 Yanga.

SOMA NA HII  KIFAA CHA MAZEMBE CHAKUTANA NA 'NKONO WA NTU' YANGA....AUMWA GHAFLA...ACHUJWA RASMI...