Home news MAJINA YA WALIOPITISHWA KUGOMBEA TFF HADHARANI LEO

MAJINA YA WALIOPITISHWA KUGOMBEA TFF HADHARANI LEO


 MCHAKATO wa uchaguzi kwa sasa bado unaendelea ambapo leo majina ya waliopenya hatua ya kugombea nafasi ndani ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, (TFF) inatarajiwa kuwa hadharani.


Kwa mujibu wa kalenda ya matukio ya uchaguzi wa TFF Juni 25-27 ni siku za kufanya usaili wa wagombea ambao walipita kwenye mchujo wa awali na zoezi hilo lilifanywa na Kamati ya Uchaguzi na wagombea wenyewe.


Jana Juni 27 ilikuwa siku ya mwisho kukamilisha mchakato huo na leo Juni 28 itakuwa ni siku ya kutangaza na kubandika kwenye mbao za matangazo matokeo ya awali ya usaili na itafanywa na Kamati ya Uchaguzi TFF.


Uchaguzi unatarajiwa kufanyika Agosti 8 ikiwa chini ya Kimoni Kibamba ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi.


Kwa upande wa nafasi ya Urais ni wagombea watatu walipitishwa kwenye mchujo wa awali ambao ni Evans G Mgeusa, Hawa Mniga na Wallace Karia ambaye anatetea kiti chake. Huku kwa upande wa wajumbe wakiwa ni 17 katika kanda 6.


Makamu Mwenyekiti wa Uchaguzi wa TFF, Benjamin Kalume alisema kuwa watasimamia haki katika uchaguzi huo kwa mujibu wa kanuni.

SOMA NA HII  BAADA YA KUONA TABIA ZAKE KUWA SIO...MORRISON APEWA MASHARTI MAPYA YANGA...NABI AKOMAA NAYE...