Dakika 90 zinakamilika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam huku Yanga wakiondoka na alama tatu muhimu.
Yanga wameitandika timu inayoburuza mkia katika msimamo wa Ligi, Mbeya Kwanza magoli 4-0.
Magoli ya Yanga Matatu yamefungwa Kipindi cha Kwanza na Fiston Mayele, Ntibazonkiza na Dickson Ambundo.
Kipindi cha Pili Mshambuliaji Heritier Makambo aliwafungia Yanga goli la nne na kuwahakikishia alama tatu.
Ushindi huo unawafanya Yanga kufikisha alama 63, huku wakihitaji alama 6 tu kujitangazia ubingwa katika michezo mitano waliyobakisha.