Home Azam FC RASMI…AZAM FC WAZIDI KUTIA MACHUNGU SIMBA SC…WAMALIZANA NA SOPU KWA DAU NONO…ALAMBISHWA...

RASMI…AZAM FC WAZIDI KUTIA MACHUNGU SIMBA SC…WAMALIZANA NA SOPU KWA DAU NONO…ALAMBISHWA MIAKA MITATU…


Kiungo mshambuliaji wa Coastal Union, Abdul Hamis Seleman “Sopu” amejiunga na matajiri wa Jiji Azam FC kwa mkataba wa miaka mitatu.

Sopu aliefanya vyema na Coastal Union msimu wa 2021/2022, alikuwa akiwindwa na vilabu kadhaa kabla ya Azam FC kuibuka wababe.

Sopu ametambulishwa mbele ya Vigogo wa Azam FC, Yusuph Bakhres na Mtendaji Mkuu Abdulkarim Amin.

Sopu alicheza mechi yake ya mwisho na Coastal Julai 2, katika mchezo wa Fainali ya Azam Sports Federation ambapo alitupia magoli matatu.

Sopu aliibuka mfungaji bora wa Michuano ya Azam Sports akifunga magoli tisa huku akitupia Hat trick mbili.

SOMA NA HII  WINGA MPYA WA YANGA KUTUA NCHINI, BAADA YA TETESI ZA MUDA MREFU