Timu ya Kipanga ya Zanzibar imetoa sare ya 1-1 na Al Hilal Wau y Sudan Kusini jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
Mchezo huo ulikuwa wa raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa hatua za awali.
Timu hizo zitarudiana Septemba 17 Uwanja wa Amaan, Zanzibar na mshindi wa jumla atasonga mbele.