Home Habari za michezo BAADA YA KUONA MWAMNYETO ‘ANAZINGUA’ KILA AKIPANGWA…KAZE AAMUA KUJIMALIZA KWA BACCA…

BAADA YA KUONA MWAMNYETO ‘ANAZINGUA’ KILA AKIPANGWA…KAZE AAMUA KUJIMALIZA KWA BACCA…

Habari za Simba

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema Ibrahim Bacca amewaongezea wigo katika machaguo ya wachezaji wa kuwatumia kwenye safu ya ulinzi.

Bacca ameonyesha utayari wa kutumika katika kikosi cha kwanza kwenye mchezo wa shirikisho dhidi ya Club Africain baada ya kuwa na kiwango kizuri katika mechi mbili zilizopita dhidi ya KMC na Geita Gold

“Bacca amecheza vizuri mechi zilizopita hili jambo jema kwake na timu kwa ujumla kwani ametuongezea ubora kwenye safu ya ulinzi”, alisema

Baada ya nahodha Bakari Nondo Mwamnyeto kukabiliwa na matatizo ya kifamilia, Bacca anaonekana kuwa kwenye nafasi nzuri ya kuanza mbele yake baada ya kuonyesha ubora katika mechi alizopewa nafasi

Dickson Job na Bacca wameonyesha ‘ukatili dhidi ya washambuliaji wa timu pinzani licha ya maumbile ya miili yao kuwa madogo.

SOMA NA HII  HUYU HAPA ATAJWA KUWA MCHEZAJI HATARI SIMBA