Home Habari za michezo KUELEKEA QATAR: SENEGAL KUTUMIA WAGANGA WA KIENYEJI KUMTIBU SADIO MANE..

KUELEKEA QATAR: SENEGAL KUTUMIA WAGANGA WA KIENYEJI KUMTIBU SADIO MANE..

BARNET, ENGLAND - MARCH 23: Sadio Mane of Senegal runs with the ball during the International Friendly match between Nigeria and Senegal at The Hive on March 23, 2017 in Barnet, England. (Photo by Dan Mullan/Getty Images)

Katibu Mkuu wa FIFA Msenegal Fatma Samoura, amesema kuwa Senegal itatumia Waganga wa kienyeji ili kuhakikisha Sadio Mané (30) anashiriki katika fainali za Kombe la Dunia 2022.

Mané alipata jeraha la tendon wakati wa mchezo wa Bayern Munich dhidi ya Werder Bremen mapema wiki hii ambalo litamuweka nje ya uwanja kwa mwezi mmoja.

Hata hivyo iliripotiwa kuwa Mané anaweza kushiriki Kombe la Dunia huku ikielezwa kuwa kocha wa Senegal Aliou Cissé anatarajia kumjumuisha katika kikosi chake atakachokitangaza siku ya Ijumaa.

“Tutatumia waganga,” amesema Somoura

Alipoulizwa juu ya ufanisi wa waganga alijibu:-

“Sijui (kama zinafaa) lakini katika hali hii, tutazitumia hivyo hivyo. Tunatumaini miujiza. Lazima awepo Qatar

SOMA NA HII  BAADA YA KUKIWASHA MECHI YA DAR....NTIBAZONKIZA AWALIA KIAPO AL AHLY MECHI YA MISRI...