Home Habari za michezo KISA YANGA KUFUNGWA…KAMWE AWASHUKIA WAANDISHI WA HABARI KWA KUIPENDELEA IHEFU…

KISA YANGA KUFUNGWA…KAMWE AWASHUKIA WAANDISHI WA HABARI KWA KUIPENDELEA IHEFU…

Afisa Habari wa Yanga SC Ally Kamwe

Afisa Habari wa Yanga SC, Ally Kamwe amewatolea uvivu waandishi wa habari kwa kusema, wameshindwa kuripoti vizuri rekodi yao ya unbeaten na badala yake, wameungana kuishangilia Ihefu iliyopata ushindi dhidi ya mabigwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kamwe ametoa kauli hiyo leo Desemba Mosi, 2022 alipokuwa akifanya mahojiano na Wasafi FM akinadi mchezo wao dhidi ya Tanzania Prisons unaotarajiwa kufanyika Jumapili hii katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.

“Unajua hamkututendea haki Yanga Africans, mlipaswa kutenga muda hata wa lisaa kujadili rekodi yetu ambayo tumeiweka, mlipaswa kuchambua kwa umakini ni rekodi ambayo sidhani kama inaweza kuwekwa tena nchini labda turudie sisi wenyewe,” alisema Ally.

SOMA NA HII  WANAOONGOZA KWA KUWA MAN OF THE MATCH MESSI NA RONALDO WACHUANA TENA...