Habari za michezo
MASTAA YANGA WATIKISA TUNISIA…TIZI LAO LAWA GUMZO KOTE…(PICHA)
Kikosi cha Yanga rasmi kimeanza mazoezi nchini Tunisia, baada ya kuwasili mjini Tunis jana Jumatano (Februari 08), kikitokea Dar es salaam-Tanzania.
Kurasa za Mitandao ya Kijamii za Yanga zimethibitisha taarifa za kuanza kwa maandalizi ya kikosi cha klabu hiyo, kwa kuweka picha za Wachezaji wakiwa Uwanja wa mazoezi.
Picha za mazoezi ya wachezaji ya Yanga imeambatana na ujumbe unaosomeka: “Tumeanza mazoezi rasmi kuelekea mchezo wetu wa kwanza #cafconfederationcup ugenini dhidi ya US Monastir Jumapili”


Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.