Habari za Simba
Habari za michezo

BAADA YA SAWADOGO KUYUMBA MECHI NA WAMOROCCO…MBRAZILI SIMBA ASHUSHA PUMZI NA UJIO WA KANOUTE…

admin February 20, 2023 9:01 pm

Kocha Mkuu wa Simba SC, Roberto Oliviera ‘Robertinho’ amesema anayo furaha kuona kiuongo wake mkabaji anakuwa sehemu ya kikosi kitakachowavaa Azam FC kesho Februari 21, 2023 baada ya kumkosa kwenye mchezo wao uliopita wa Kimataifa dhidi ya Raja Casablanca akitumikia adhabu ya kadi tatu za njano.

Robertinho amesema, alimkosa nyota huyo kwenye mchezo huo muhimu ambao alipoteza kwa goli 3-0 lakini sasa anakwenda kumtumia kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC ambayo anaamini itakuwa na ‘aproch’ tofauti.

“Ni furaha kwangu kumuona anarejea baada ya kukosa mchezo uliopita, anakwenda kuniongezea wigo mpana wa kufanya uchaguzi wa mtu wa kucheza kwani wanakuwa sasa wachezi wawili au watatu kwenye nafasi yake,” alisema Robertinho.

Simba SC wanawakaribisha Azam FC kesho kwenye dimba la Benjamini Mkapa wakiwa nafasi pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC na pointi zao 53 huku Azam wao wakiwa nafasi ya nne na pointi zao 43.

MAYELE AFICHUA WALICHOWAFANYIA WACHEZAJI WA MAZEMBE WAKATI MECHI IKIENDELEA JANA… KISA YANGA KUICHAPA MAZEMBE JANA…NABI AWAPIGA KIJEMBE SIMBA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply