Azam FC
AZAM FC YATISHIWA USALAMA…MECHI DHIDI YA GOR MAHIA KUSITISHWA
Marce Ben Komba
March 22, 2023
6:29 pm
Klabu ya Azam FC imesitisha safari yake ya Kenya kwenda kucheza na Gor Mahia Jumapili hii, kutokana na sababu za kiusalama.
Azam FC, mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na Kombe la Kagame, walialikwa na wababe hao wa Kenya, Gor Mahia kwa ajili ya mchezo huo wa kimataifa wa kirafiki uliopangwa kufanyika Uwanja wa Nyayo Jijini Nairobi.
Hata hivyo, mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya JKU ya Zanzibar utafanyika kama ilivyopangwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex saa 1.00 usiku.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.