Home Habari za michezo AHMED ALLY:- KIKOSI CHA PILI CHA SIMBA KWA MTIBWA NDIO KIKOSI CHAO...

AHMED ALLY:- KIKOSI CHA PILI CHA SIMBA KWA MTIBWA NDIO KIKOSI CHAO CHA KWANZA….

Habari za Simba SC

Kuelekea Mchezo wa Mtibwa Sugar na Simba SC, Afisa Habari wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally, amefunguka juu ya kikosi chao kuelekea mchezo huo huku akisema kuwa Kikosi cha pili cha Klabu yake ndio kikosi cha Kwanza cha Mtibwa Sugar.

Akizungumza kupitia Radio EFM mapema hii leo, Ahmed Ally alisema anaamini kabisa mchezi wa kikosi cha pili, akienda Mtibwa anakuwa wa kikosi cha kwanza.

“Kikosi cha pili cha Simba ndio kikosi cha kwanza cha Mtibwa Sugar, mchezaji wetu akienda Mtibwa anakuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza na wa kutumainiwa mfano ni kijana wetu Duchu na amepewa unahodha,” alisema Ahmed Ally.

Mtibwa Sugar kesho itakuwa ikiwakaribisha Simba SC kwenye Uwanja wa Manungu mjini Morogoro katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC.

SOMA NA HII  MAGAZETI: USAJILI MPYA SIMBA UNATISHA...NABI AFUATA DAWA YA TP MAZEMBE