ZA NDANII KABISA...MECHI SIMBA NA YANGA...MAREFA WOTE WANAWAKE
Habari za michezo

ZA NDANII KABISA…MECHI SIMBA NA YANGA…MAREFA HAWA WOTE WANAWAKE

Marce Ben Komba April 14, 2023 2:42 pm

Hii ni mara ya kwanza katika historia ya mchezo wa dabi kuonekana safu nzima ya waamuzi kuwa jinsi ya kike kuhakikisha dakika 90 zinamalizika salama.

Inadaiwa kuwa kamati ya waamuzi ilishamaliza kuteua majina ya waamuzi hao kitambo sana tena wote wenye hadhi ya Fifa lakini kutokana na ukubwa wa mchezo kuna safu nyingine ya watu wanatakiwa kuwekwa.

Chanzo kutoka kamati ya waamuzi kinaeleza wao walishamaliza kazi yao ya kuteua majina kisha kuyawakilisha TFF kwa ajili ya mambo mengine ikiwa pamoja na kuyatangaza.

“Majina yote ya waamuzi nayafahamu lakini kimaadili siwezi kukutajia japo tulitarajia hadi muda huu yangekuwa yametangazwa hivyo sijui kinachokwamisha maana huu ni mchezo mkubwa,” kinaeleza chanzo hicho.

Chanzo kingine kutoka ndani zaidi kinadai mwamuzi wa kati atasimama, Jonesia Rukyaa, wamuzi wa pembeni yupo, Janeth Balama na mmoja kati ya Zawadi Yusuph na Glory Tesha kama hakutakuwa na mabadiliko.

Waamuzi wa akiba (official) anaweza akawa, Tatu Malogo au Ester Adalbert lakini tayari lugha gongani imeanza kujitokeza huko ndani.

“Kuna wengine walitaka, Tatu ndio asimame kati lakini Jonesia ndio anaonekana kukubalika zaidi, ugumu unakuja kati ya Zawadi pamoja na Glory hapo ndio kuna mgawanyiko nani apewe nafasi.” anasema mtoa taarifa.

Hata hivyo anasema majina ya waamuzi yatatangazwa muda wowote kuanzia leo Ijumaa, Aprili 14 baada ya taratibu nyingine kukamilika.

SIKU ZA JOB ZAHESABIKA YANGA…AGOMA KUSAINI MKATABA MPYA…UTATA MZITO WAIBUKA IMEVUJA!! MABOSI SIMBA WAMWAGA MANOTI…WAIFUNGIA KAZI YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply