IMEVUJA!! MABOSI SIMBA WAMWAGA MANOTI...WAIFUNGIA KAZI YANGA
Habari za michezo

IMEVUJA!! MABOSI SIMBA WAMWAGA MANOTI…WAIFUNGIA KAZI YANGA

Marce Ben Komba April 14, 2023 2:54 pm

Mabosi wa Simba wameamua kuifungia kazi Yanga inayonolewa na Kocha, Nasreddine Nabi kwani wamesema hawataki chochote zaidi ya ushindi katika Kariakoo Dabi, ambapo tayari wameandaa bonasi ya kutosha ya zaidi ya Sh 300 Milioni kwa wachezaji ili kufanikisha ushindi jumapili.

Katika mchezo huo, Simba wataingia wakiwa na hasira ya kufungwa mara mbili mfululizo walizokutana katika Ngao ya Jamii msimu huu na uliopita.

Taarifa zinasema mabosi hao wa Simba kitu pekee ambacho wanakitaka katika msimu huu ni kuifunga Yanga, hiyo ni baada ya kushindwa kuifunga kwa misimu miwili.

Mtoa taarifa huyo alisema kuwa mabosi hao wa Simba, wameweka nguvu hizo za kuwafunga Yanga kwa ajili ya kuwapa furaha mashabiki wao.

ZA NDANII KABISA…MECHI SIMBA NA YANGA…MAREFA HAWA WOTE WANAWAKE MMH HII SASA KUFURU…MABOSI WA SIMBA WAINGIA KAMBINI NA TIMU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply