Habari za michezo
“KANOUTE ANASUMBULIWA NA NYONGA…SIMBA WASHINDWA KUVUMILIA WAFUNGUKA HAYA
Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wameeleza kilichomfanya nyota wao Sadio Kanoute akosekane kwenye mchezo wa dabi dhidi ya Yanga SC pamoja na mechi nyingine zilizotangulia zikiwemo mbili dhidi ya Ihefu FC.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 18, 2023, Afisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally, alisema, Kanoute alipata majeraha ya nyonga hivyo ataingia kambini leo na kisha kufanyiwa vipimo kujua kama anaweza kuendelea na mazoezi au la.
“Kanoute, anasumbuliwa na nyonga, atakutana na madaktari leo kujiridhisha kama yupo fiti ataanza mazoezi,” alisema Ahmed.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.