Habari za Simba
Habari za michezo

KUHUSU ISHU YA KANOUTE….SIMBA SC WAVUNJA UKIMYA KUHUSU YANAYOENDELEA JUU YAKE…

admin April 19, 2023 6:54 pm

Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wameeleza kilichomfanya nyota wao Sadio Kanoute akosekane kwenye mchezo wa dabi dhidi ya Yanga SC pamoja na mechi nyingine zilizotangulia zikiwemo mbili dhidi ya Ihefu FC.

Akizungumza na waandishi wa habari , Afisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally, alisema, Kanoute alipata majeraha ya nyonga hivyo ataingia kambini leo na kisha kufanyiwa vipimo kujua kama anaweza kuendelea na mazoezi au la.

“Kanoute, anasumbuliwa na nyonga, atakutana na madaktari leo kujiridhisha kama yupo fiti ataanza mazoezi,” alisema Ahmed.

Ahmed alisema, mwingine ambaye alikuwa majeruhi ni golikipa namba moja Aishi Manula ambaye naye leo atawasili kambini na madaktari wataangalia, kama tatizo lake linaweza kupona lenyewe au atahitajika kufanyiwa upasuaji.

Kuhusu Agustine Okrah, Ahmed alisema alishapona siku nyingi, alianza mazoezi lakini hakuwa fiti kuanza dhidi ya Yanga hivyo anaendelea na mazoezi.

BAADA YA KICHAPO CHA SIMBA…NABI AFUNGUKA HAYA..AMTAJA AZIZ KI HUYU HAPA STAA WA BONGO FLEVA ALIYEPEWA SHAVU NA SERGIO RAMOS WA PSG….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply