
Vile vile aliwashukuru wadau wa mashirika na makampuni mbali mbali kama Sanlam, Jubilee General Insurance, Garda World, Cheknocrafts, Icea Lions Insurance, Metropolitan Life Insurance, Strategies Insurance, Hans Paul, SBC- Pepsi, na Aramex kwa udhamini wao ili kufanikisha mbio hizi.
Kwa Upande wake Mkurugenzi wa programu kutoka Benjamin Mkapa Foundation alisema. “Nina furaha kujumuika na NBC katika mbio hizi kwani fedha zitakazo patikana katika mbio hizi zitasaidia kusomesha wakunga zaidi na kuboresha huduma ya afya kwa mama na mtoto na hivyo kujenga taifa lenye afya bora, Tatizo hili ni kubwa na uhaba wa wataalamu hawa ni mkubwa hivyo tunawasihi watanzania kujumuika katika mbio hizi kuchangia upatikanaji wa fedha ili tuweze kukabiliana na uhaba huu kwa pamoja” alisema.