Habari za michezo
MASHINE YA KAZI HII HAPA….MABOSI SIMBA NA YANGA WAVIZIANA AIRPORT…
admin
May 26, 2023
8:42 pm
Beki wa Kati wa Kabwe Warrior ya Zambia, Marcel Kalonda raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo anahusishwa na klabu zenye misuli ya kiuchumi Tanzania [Singida Big Star, Simba, Yanga na Azam FC].
Baada ya kuonesha kiwango kikubwa kwenye Ligi ya Zambia kwa kutwaa mataji manne ya Ligi hiyo akiwa na Zesco United ikiwa ni pamoja na kucheza Robo Fainali mbili mfululizo za Ligi ya Mabingwa Afrika [2018|19 na 2019|20].
Wakati msimu unaelekea mwishoni, tayari baadhi ya klabu zimeanza mipango ya kuimarisha vikosi vyao baada ya kuona mapungufu yakiyojitokeza kipindi chote cha msimu huu.
Endapo Marcel Kalonda atafanikiwa kutua Tanzania ataungana na wachezaji wengi raia wa DR Congo wanaocheza Ligi Kuu na Ligi ya Championship.
Post Views: 1
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.