Birmingham City vs Southampton
Meridianbet

Birmingham City dhidi ya Southampton Uso kwa uso Championship

Vardo September 1, 2026 1:26 pm

Uwanja wa St. Andrew’s @ Knighthead Park utakutanisha mchezo wa raundi ya nne ya Championship kati ya Birmingham City na Southampton Leo Jumanne, tarehe 1 Septemba 2026, saa 22:00 usiku, Mechi hii inayojulikana kama “Hollywood Derby” kutokana na wamiliki maarufu wa Birmingham, inakutanisha timu mbili zilizorudi hivi karibuni katika ligi ya championship.

 

Birmingham City wanaingia kwenye mechi hii wakiwa hawajafungwa katika mechi tatu za kwanza za Championship, huku wakiwa nafasi ya nane kwenye msimamo na pointi tano. Walianza msimu kwa sare bila mabao dhidi ya Sheffield United, kisha wakatoka sare 2-2 dhidi ya Bristol City nyumbani.

 

Baada ya kupata kipigo cha mabao 6-1 dhidi ya Brentford wa Premier League kwenye Kombe la EFL, timu ya kocha Chris Davies ilionyesha nguvu kwa kuwafunga wapinzani wao wa kwenye championship, Wrexham, kwa mabao 2-1.

 

Kwa upande wa Southampton, msimu haukuanza vizuri kwani walikabiliwa na adhabu ya kupunguziwa pointi nne kwa msimu wa 2026-27 kutokana na tukio la “Spygate” kurekodi mazoezi ya wapinzani bila idhini.

 

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema.  Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

 

Hata hivyo, timu hiyo chini ya kocha Eckert Tonda imeonyesha uwezo mkubwa hivi karibuni, ikiwapiga Millwall mabao 5-1 baada ya kuanza msimu kwa kufungwa. Katika ushindi huo, mabao yalipatikana kupitia Tom Fellows, Leo Scienza, Finn Azaz, na Cyle Larin aliyefunga mara mbili.

 

Historia ya michezo kati ya timu hizi mbili inaonyesha Southampton wakiwa na ubora mkubwa, wakiwa wameshinda mara 18 dhidi ya ushindi 12 wa Birmingham katika mechi 40 za awali, huku mechi 10 zikiisha sare.

 

Aidha, Southampton hawajafungwa dhidi ya Birmingham katika mikutano sita ya mwisho, wakiwa na ushindi minne pamoja na sare mbili. Msimu uliopita, mechi ya Birmingham iliisha sare 1-1, wakati Southampton walishinda 3-1 katika mchezo wa nyumbani St. Mary’s.

 

Kwa mtazamo wa kimbinu, Birmingham watahitaji kudhibiti kwa karibu wachezaji kama Iwata na Solis, huku wakimzuia Finn Azaz nafasi kati ya eneo la ulinzi na kati. Southampton kwa upande wao wanatarajiwa kubana mchezo wa kujenga wa Birmingham kabla ya kushambulia kwa kasi kupitia Matsuki na Scienza, huku mipira ya kusimama ikiwa muhimu iwapo James Ward-Prowse ataanzia.

Barker Afichua Sababu ya Kumtoa Libasse Gueye Dhidi ya Geita Gold Bonasi, Tumble Na X100, Meridian Bonanza Yazidi Kupandisha Joto