Habari za Simba SC
Habari za michezo

FAILI LA MASTAA WAPYA NA WATAKAO TEMWA SIMBA HILI HAPA….MBRAZILI ‘KAKAZA SHINGO’ AISEE..

admin May 31, 2023 10:36 am

Taarifa za ndani kutoka Klabu ya Simba zinaeleza kuwa, ripoti ya Kocha Mkuu, Roberto Oliveira kwa bodi ya wakurungezi wa klabu hiyo inataka usajili wa wachezaji nane wapya ikiwa wachezaji watano wa kimataifa na wachezaji watatu wawe wachezaji wa ndani.

Katika ripoti hiyo Robertinho ametaka golikipa, beki wa kushoto, beki wa kati, viungo wawili, winga mmoja na washumbuliaji wawili.

Katika mapendekezo yake, Mbrazil huyo katika wachezaji watano wapya wa kimataifa anaowataka (golikipa mmoja, beki wa kati mmoja, kiungo wa kati, winga na mshambuliaji mmoja).

Aidha, Robertinho ametaka wachezaji watatu wa ndani (ambao ni beki wa kushoto, kiungo wa kati na mshambuliaji mmoja).

Kwenye ripoti hiyo Robertinho anataka wachezaji wanaocheza timu zao za taifa na wawe kwenye kikosi cha kwanza kwenye timu wanazotoka.

Pia, kocha huyo amependekeza kuachana na wachezaji Mohamed Ouattara, Agustine Okrah, Peter Banda, Ismail Sawadogo, Gadiel Michael, Beno Kakolanya na Habibu Kyombo wakati Peter Banda akiomba kuondoka klabuni hapo kwa mkopo.

Katika hatua nyingine, kocha huyo ameomba wachezaji wawili wa kimataifa Pape Ousmane Sakho na Joash Onyango wasiondoke klabuni hapo, hii ni baada ya wachezaji hao kuomba kuondoka Simba SC.

Wachezaji wa kimataifa wenye uhakika wa kuendelea kubaki Simba kwa msimu ujao 2023/24 ni beki Henock Inonga Baka, viungo Sadio Kanoute, Clatous Chama na Saido Ntianzokiza na washambiaji Moses Phiri na Jean Baleke.

Pamoja na hayo, Robertinho ameomba kuongezewa watu kwenye bechi la ufundi ili kuifanya kuimarisha zaidi benchi la msimu huu.

MAYELE KULIPWA MIL 53 KWA MWEZI…YANGA KULAMBA MABILIONI…SIMBA WAFUATA BEKI IVORY COST.. KUHUSU ISHU YA TSHABALALA KUKATAA OFA MIL 400 NA MSHAHARA WA MIL 30 KUTOKA SAUZI..UKWELI HUU HAPA..

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply