Habari za Simba
Habari za michezo

BAADA YA KUTEMWA JANA….AKPAN NAYE KAONA ISIWE TABU….ONA ALIYOYASEMA KWA MABOSI WA SIMBA…

admin June 22, 2023 7:30 am

Uongozi wa Simba ilitangaza kuachana na kiungo Mnigeria Victor Akpan ambaye alijiunga na timu hiyo Julai 2022 kutoka Coastal Union,kwa mkataba wa miaka miwili.

Akpan ametumikia mkataba wake kwa mwaka mmoja akitumia nusu msimu Simba na nusu Ihefu alipoenda kwa mkopo.

Akpan kupitia akaunti yake ya Instagram amewashukuru viongozi na mashabiki wa Simba na Klabu imemfanya kuwa imara na jasiri

“Napenda kutumia fursa hii kuwashukuru mashabiki wote wa klabu ya Simba na Uongozi wote kwa nafasi nzuri ya kuwa sehemu ya familia kubwa katika kipindi changu kwenye klabu, kwa kweli haikuisha kama nilivyotarajia lakini kuna mengi nimejifunza”.

“kucheza katika klabu hii kumenifanya niwe imara na mwenye kujituma zaidi, jasiri na nimebaki na kumbukumbu ,nzuri moyoni mwangu”.

“Kama inavyosemwa kila chenye mwanzo pia kina mwisho wa awamu nyingine, Mungu awabariki wote”

Kiungo huyo alisajiliwa kwenye dirisha kubwa la usajili msimu huu na alitolewa kwa mkopo kwenda Ihefu kwenye dirisha dogo la usajili msimu 2022/23..

Tayari Simba imeachana na wachezaji wawili wa kigeni ambao ni Akpan na Augustine Okrah.

NOGESHA USHINDI WAKO KWA KUCHEZA PLANET POWER YA MERIDIANBET CASINO… KUHUSU ISHU YA KUTUA SIMBA ….SAMATTA KATIKISA KICHWA KISHA AKASEMA HILI JIPYA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply