Habari za michezo
WAKATI ISHU YA MAYELE IKIWA KIZUNGUMKUTI….MPOLE ANUKIA YANGA…AKUTANA NA MABOSI KUYAJENGA…
admin
July 10, 2023
6:45 pm
Mshambuliaji wa FC Lupopo ya DR Congo, George Mpole ameamua kubadili gia akiwa angani, licha ya kuwa alishakubaliana kila kitu na klabu ya Kitayosce ila sasa akili yake ipo Jangwani.
Siku ya Alhamisi alionekana na Bosi Mkubwa wa klabu ya Yanga huku akionekana mwenye furaha.
Huenda akawa mbadala na Hafiz Konkon ambaye Yanga SC wanazungumzwa kumtaka na huenda wakaamua kuachana nae.
Pia kutua kwa Mpole Yanga Sc inaonyesha kuna mshambuliaji mzawa ataondolewa pale, iwe kutolewa kwa mkopo ama kuvunjiwa Mkataba.
George Mpole kabla ya kwenda zake Congo alikuwa mfungaji Bora wa Ligi Kuu kwa msimu wa 2021/22 amabpo alimfunika Mayele kwa kumzidi goli moja.
Washambuliaji wa kati (Mambo yakikaa sawa)
Fiston Mayele
Clement Mzize
Kennedy Musonda
Yusuph Athuman
George Mpole
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.