Habari za Yanga leo
Habari za michezo

PAMOJA NA KUSEPA ZAKE BONGO….HIVI NDIVYO YANGA INAVYOZIDIA KUMPAISHA NABI KIMATAIFA…

admin July 11, 2023 9:28 pm

Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya Yanga SC ,Nasreddine Nabi ameorodheshwa na Mtandao wa Foot-African.com kwenye orodha ya Makocha waoanowania Tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka wa Afrika.

Msimamo ulivyo mpaka sasa

1. Walid Regragui (Morocco): 36%

2. Aliou Cissé (Sénégal): 29%

3. Abdelhak Benchikha (USM Alger): 21%

4. Nasreddine Nabi (Young Africans): 13%

Nabi akiwa Kocha wa Yanga msimu uliopita alikuwa na mafanikio makubwa akibeba Ngao ya Jamii, Kombe la Azam Sports Federation, Ligi Kuu na kufika Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Nabi kwa sasa hana timu baada ya kuachana na Klabu ya Yanga mwishoni mwa msimu uliopita, awali alihusishwa na dili la kwenda kuwa kocha mkuu wa Kaizer Chiefs kabla ya dili hilo kutibuka dakika za jioni.

Hata hivyo bado kocha huyo mwenye misimamo anatajwa kuwaniwa na klabu nyingi za Uarabuni ikiwemo Misri na kwao Tunisia.

Mwananchi unaweza kumpigia kura Nasreddine Nabi?

WAKATI SIMBA NA AZAM WAKISHUSHA VIFAA VYAO…ENG HERSI KATIKISHA KICHWA KISHA AKASEMA HAYA… HUU HAPA UKWELI WA DILI LA NGOMA NA SIMBA…KWANINI HAJATAMBULSIHWA MPAKA SASA ..?

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply