Habari za michezo
YANGA HAIBOI, HAIPOI, YATAMBULISHA BEKI MPYA KUTOKA ASEC MIMOSAS
Staff Desk
July 15, 2023
4:51 am
KLABU ya Yanga imemtambulisha beki wa kulia, Kouassi Attohoula Yao (26) kuwa mchezaji wake mpya wa tano kutoka ASEC Mimosas ya kwao, Ivory Coast.
Wachezaji wengine wapya wa kigeni Yanga ni winga Maxi Mpia Nzengeli kutoka Maniema ya kwao, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na beki wa kati Gift Freddy kutoka SC Villa ya kwao, Uganda.
Yanga pia imesajili wazawa wawili, beki wa kushoto Nickson Kibabage kutoka Singida Fountain Gate na kiungo Jonás Mkude kutoka kwa mahasimu, Simba SC.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.