Habari za michezo

ALIYEKUWA KOCHA WA YANGA, NABI ATUA FAR RABAT YA MOROCCO

Staff Desk July 18, 2023 10:30 am

Aliyekuwa kocha wa Yanga Nasreddine Nabi amesaini mkataba wa miaka miwili kuwafundisha Mabingwa wa Ligi Kuu ya Morocco FAR Rabat.

Nabi amesaini mkataba huo jana kuwafundisha Mabingwa hao wa msimu huu nchini humo ikiwa ni miezi michache tangu aachane na Yanga.

Nabi amesema ni heshima kwake kupata nafasi ya kuifundisha klabu hiyo kubwa Afrika ambapo anataka kuhakikisha anatumia taaluma yake kuipa mafanikio zaidi.

“Ni changamoto mpya kwangu, FAR Rabat ni klabu kubwa Afrika kunipa nafasi ya kufanya kazi hapa ni heshima kubwa kwangu,naamini ni wakati mzuri kwetu kushirikiana kuipa mafanikio zaidi klabu hii,”amesema Nabi.

Akiwa Yanga Nabi ameiacha timu hiyo ikiwa na heshima kubwa akiwapa mataji yote ya ndani kwa misimu miwili mfululizo lakini pia msimu uliopita akiifikisha kucheza Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

ISHU YA KOCHA WA SIMBA KUONDOKA KAMBINI IKO HIVI…. ROBERTINHO AFUNGUKA KILA KITU MKUDE:- ROHO YANGU ILIKUWA YANGA TU….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply