ayoub
Habari za michezo

SIMBA YAMTAMBULISHA KIPA WAKE MPYA KUTOKA MOROCCO

Staff Desk August 12, 2023 2:33 pm

Klabu ya Simba imethibitisha kukamilisha usajili wa kipa, AYOUB LAKRED kutoka FAR Rabat ya Morocco kwa Mkataba wa miaka miwili.

Lakred (28) ameiongoza FAR Rabat kushinda ubingwa wa Ligi Kuu ya Morocco na kuifikisha Nusu fainali ya CAFCC.

Lakred anakuja Tanzania na medali ya ubingwa wa Ligi kuu ya Morocco aliyoivaa wiki kadhaa zilizopita.

Anakuja na kumbukumbu ya mwisho ya Kimataifa kwake ni kucheza robo fainali ya Kombe la Shirikisho Africa akiwa na AS Far Rabat.

Amekuja Kipa aliyekua akiitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Morocco inayocheza fainali za CHAN.

GAMONDI ATAMBA, YANGA BADO HAWAJAANZA KUTUMIA MIFUMO YAKE ROBERTINHO ATETA NA WACHEZAJI WAKE KABLA YA KUKUTANA NA YANGA KESHO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply