Habari za michezo

UNAAMBIWA MTIBWA SUGAR WAAMKA NA SIMBA SC…. ISHU IKO HIVI

Staff Desk August 16, 2023 12:50 pm

Timu ya Mtibwa Sugar kutoka Morogoro, imetamba kuibuka na ushindi katika mchezo wao wa ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2023/24 dhidi ya Simba SC ya Dar es salaam.

Mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, utapigwa Alhamis (Agosti 17), huu kwenye Uwanja wa Manungu uliopo Turiani mkoani Morogoro.

Afisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru, amewataka wapinzani wao hao kujiandaa kisaikolojia na mchezo huo kwani matokeo watakayoyapata hawatayaamini.

Kifaru ameongeza kuwa, anafahamu mchezo huo utakuwa mgumu kwani Simba SC watataka kupata ushindi, lakini na wao wamejiandaa vizuri, hivyo watahakikisha wanaibuka na alama zote tatu.

“Tunawaambia hao Simba SC wasitarajie mteremko kutoka kwetu kwenye mchezo huo, ule unyonge tuliouonesha msimu uliopita hautotokea msimu huu, kwa sasa tupo ngangari,” amesema Kifaru.

SIMBA SC YAANIKA MIPANGAO YAKE HII WAZI 2023/24 WAKATI ‘SKUDU’ AKIRUDI ….TFF NAO WAANZA KUFANYA YAO KWA YANGA….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply