Habari za michezo
SIMBA WANAJAMBO LAO LEO, KIVUMBI LIGI KUU
Staff Desk
August 17, 2023
12:34 pm
MIAMBA ya soka nchini Simba, leo inaanza kampeni ya kusaka ubingwa wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa Sugar.
Mchezo huo pekee leo wa ligi hiyo utafanyika kwenye uwanja wa Manungu Complex, Turiani mkoa wa Morogoro.
Ligi hiyo imeshuhudia michezo miwili Agosti 16, Azam ikiifunga Tabora United mabao 4-0 na Mashujaa ikiichapa Kagera Sugar mabao 2-0.
Hata hivyo, mchezo wa Azam na Tabora United ulishindwa kuendelea baada ya wachezaji wawili wa Tabora UTD kuumia na kufanya wabakie sita uwanjani na hivyo mchezo kukosa sifa kikanuni kuendelea.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.