Habari za Simba SC
Habari za michezo

SIMBA WAITAMANI COASTAL UNION….. ISHU YAFIKA BODI YA LIGI

Staff Desk August 23, 2023 10:37 am

Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wamekiri kuwaandikia bodi ya Ligi barua ya kuomba wacheze raundi ya tatu mechi dhidi ya Coastal Union.

Akizungumzia suala hilo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema Bodi ya Ligi waliuweka ‘pending’ mchezo huo wakidhani Simba wataanzia hatua ya awali katika michezo ya Kimataifa lakini bahati nzuri hawakuanzia.

“Ilikuwa tusicheza raundi ya tatu kutokana na kudhani tutaanzia hatua ya awali Klabu Bingwa lakini bahati nzuri hatukuanzia hatua hiyo.

“Ukiangalia ratiba tuna mchezo mwingine tarehe tatu mwezi wa kumi. Tumeomba watupe mechi na Coastal Union ili kuepuka viporo huko baadaye. Bodi nadhani wataangalia na wenzetu nafasi yao ili kama wana nafasi nzuri basi tutacheza watakapoturuhusu, sisi tupo tayari na ndio maana tukaomba tupangiwe wiki hii,” alisema Ahmed.

UTATA KWISHA…. BABA: MSUVA ANASAINI HAPA….. KIVULI CHA NABI CHAMTESA GAMONDI YANGA ROBERTINHO AFUNGUKA KUHUSU SOKA ANALOLITAKA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply