Home Habari za michezo MCHAMBUZI: SIMBA IMEBEBWA NA YANGA KIMATAIFA….

MCHAMBUZI: SIMBA IMEBEBWA NA YANGA KIMATAIFA….

Yanga SC na Simba SC

Wakati Simba ikiwa inafanya makubwa katika michuano ya CAF barani Afrika ikiwemo kushiriki Michuano ya African Super Cup (African Football League).

Mchambuzi wa Michezo kutoka Clouds Media Master Tindwa ameyatazama mafanikio hayo ya Simba kuwa yamebebwa zaidi na Klabu ya Yanga.

Akifafanua hilo Master Tindwa anasema;

“ Haina haja ya kung’ata maneno Yanga ndio klabu kubwa Tanzania, ki-umri hata mataji. Simba ni wakubwa nje hasa kwa kipindi hiki cha miaka 5 iliyopita, hata kucheza Super league hawachezi kwa bahati mbaya, ”

“ Mi nadhani Simba wamenufaika kupitia Yanga, wameitumia kama Case study kwenye tamasha lililopipa wakafanyia kazi pale Yanga walipokosea ndio maana unaona watu wengi wamejitokeza kununua tiketi.. Lakini tukumbuke kuna maisha baada ya matamasha, ”

SOMA NA HII  KIPIGO CHA JANA CHAZIDI KUWAZUZUA WAARABU...WAMSHITAKI MWAMUZI CAF..WADAI ALIHONGWA NA SIMBA...