Habari za michezo
NGEREZA AWALIPUA SIMBA……… LABDA YANGA LAKINI SIMBA HAWATOBOI
Staff Desk
September 18, 2023
11:28 am
Baada ya Simba kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Power Dynamos ya Zambia mchezo wa mtoano mkondo wa kwanza kuwania kufuzu hatua ya Makundi Ligiu ya Mabingwa Afrika.
Mchambuzi wa michezo kutoka TV3, Alex Ngereza amesema kwa kiwango walichokionesha Simba haini kama watafuzu kwa hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.
Akizungumza Ngereza anasema;
“Yanga wameenda na Coaster za harusi lakini wameshinda na timu ambayo mashabiki wake wameenda na Mabasi hawajashinda hii ni aibu na kujitamba kote tunaenda na gari za maana kumbe wanaenda kupata sare.
Sidhani kama Simba wanaweza wakafuzu kwenda makundi kwa kiwango ambacho wamekionyesha dhidi ya Power Dynamo ila Yanga wana uhakika wa kufuzu kwa asilimia 90 mpaka Sasa”
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.