Habari za michezo
JEMEDARI SAID:- WACHEZAJI WA SIMBA HAWAJITUMI…YANGA NI TOFAUTI KABISA…
admin
September 20, 2023
2:18 pm
Wakati Yanga ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini, Watani zao Simba SC walilazimishwa sare ya Mabao 2-2 dhidi ya Power Dynamos kutoka Zambia katika Uwanja wa Levy Mwanawasa.
Sasa mchambuzi wa michezo kutoa kituo cha redio cha EFM. Jemedari Said amesetoa maoni yake kuhusiana na sare hiyo.
Akizungumza Jemedari Said amesema;
“Simba wana wachezaji wengi bora kimbinu, lakini hawajitumi. Yanga ukiwaangalia wanavyocheza wakiwa hawana mpira,ni tofauti wanavyocheza Simba wakiwa hawana mpira. Simba ni wavivu,”
“Wanawapa (wapinzani) muda mwingi wa kuwa na mpira. Nafasi hiyo (mpinzani) hawezi kuipata kwa Yanga kwa sababu anakuwa kwenye Presha, anakabwa.”
“Yanga kwani timu yao inakaba vizuri na hawatoi muda na nafasi kwa mpinzani anapokuwa na mpira.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.