Habari za michezo
BALEKE AWEKA WAZI IDADI HII YA MABAO ANAYOYATAKA
Staff Desk
September 25, 2023
12:33 pm
Mshambuliaji wa Klabu ya Simba, Jean Baleke amesema kuwa anatamani kufunga Mabao kuanzia 20 kwenye ligi kuu msimu huu huku akimini yatatosha kuisaidia Simba kutwaa Ubingwa.
Baleke amesema hayo mara baada ya kufunga mabao matatu kwenye mechi dhidi ya Coastal Union na kufanikiwa kuongoza kwenye orodha ya mabao Ligi Kuu akiwa na mabao 5.
“Natamani kufunga mabao kuanzia 20 na kuendelea,nafahamu ni ngumu lakini kama nitapata nafasi ya kucheza naamini nitafunga zaidi na zaidi.
“Kingine huwa ni majeruhi kama yatakuwa mbali na mimi naamini nitafunga Kuanzia mabao 20 na kuendelea,mabao hayo naamini yatakuwa msaada mkubwa kwa timu kutwaa ubingwa msimu huu wa ligi ambayo ndio kiu yetu,” alisema Baleke.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.