Habari za Simba leo
Habari za michezo

BALEKE AWEKA WAZI IDADI HII YA MABAO ANAYOYATAKA

Staff Desk September 25, 2023 12:33 pm

Mshambuliaji wa Klabu ya Simba, Jean Baleke amesema kuwa anatamani kufunga Mabao kuanzia 20 kwenye ligi kuu msimu huu huku akimini yatatosha kuisaidia Simba kutwaa Ubingwa.

Baleke amesema hayo mara baada ya kufunga mabao matatu kwenye mechi dhidi ya Coastal Union na kufanikiwa kuongoza kwenye orodha ya mabao Ligi Kuu akiwa na mabao 5.

“Natamani kufunga mabao kuanzia 20 na kuendelea,nafahamu ni ngumu lakini kama nitapata nafasi ya kucheza naamini nitafunga zaidi na zaidi.

“Kingine huwa ni majeruhi kama yatakuwa mbali na mimi naamini nitafunga Kuanzia mabao 20 na kuendelea,mabao hayo naamini yatakuwa msaada mkubwa kwa timu kutwaa ubingwa msimu huu wa ligi ambayo ndio kiu yetu,” alisema Baleke.

JEAN BALEKE ALAMBA SHAVU HILI SIMBA KANOUTE HALIMBAYA, APUMZISHWE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply