Habari za Simba
Habari za michezo

KANOUTE HALIMBAYA, APUMZISHWE

Staff Desk September 25, 2023 4:45 pm

Mchambuzi wa masuala ya soka nchini kutoka East Africa Radio, Samwel Rashid mwenyewe anajiita Wakanda Republic amesema kuwa wachezaji wengi wa Klabu ya Simba SC, wamechoka kwa sababu ya kutumika kwa muda mrefu bila kupumzika.

Wakanda amesema hayo akimtolea mfano Sadio Kanoute raia wa Mali kuw amechoka zaidi tofauti na kazi aliyokuwa kiifanya msimu uliopita ndani ya kikosi hicho.

“Mwalimu anahitajji utimamu wa wachezaji, mwalimu anahitaji utayari wa miili ya wachezaji, miili ya wachezaji wa Simba waliokuwepo msimu uliopita fatigue (uchovu) upo ndani ya miili yao, angalia work-rate aliyokuwa nayo Kanoute msimu uliopita halafu mwangalie Kanoute wa msimu huu.

“Huwezi kusema ni mchezaji mbovu lakini ile spirit ya upambanaji aliyokuwa nayo msimu uliopita na msimu huu unaona kabisa kuna namna imepungua, kwa sababu ni mchezaji ambaye amekuwa akitumika mfululizo kwa misimu karibia miwili mfululizo day in-day out unamuona Kanoute uwanjani,” Wakanda Republic.

BALEKE AWEKA WAZI IDADI HII YA MABAO ANAYOYATAKA CHAMA ALAMBA DILI LA KIBABE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply