Afisa Habari wa Yanga SC Ally Kamwe
Habari za michezo

YANGA WAFUNGUKA KUHUSU SKUDU, NI JAMBO LA MUDA TU

Staff Desk September 26, 2023 12:00 pm

Yanga SC wamesema Mahlatse Makudubela Manoka ‘Skudu’ yupo na muda ukifika wa kucheza basi Wanayanga watamuona uwanjani akiitumikia klabu yake.

Akizungumza na Wasafi FM, Afisa Habari wa Yanga Ally Kamwe alisema, Skudu alipata majeraha wakati alipofika hivyo amelazimika kuanzia chini kimazoezi.

“Yanga imesajili wachezaji 28, wacheza wanaocheza ni kumi na moja na wale saba wa benchi. Skudu alipokuja alipata jeraha la goti na akakaa karibu wiki tatu hivi na kama unavyojua majeraha ya goti sio rahisi kurudi haraka uwanjani, lazima aanze taratibu na muda utafika atakuwa fiti,” alisema Ally Kamwe.

MGUNDA,ROBERTINHO WAIRARUA DYNAMO KUMBE KONKANI KWA GAMONDI BADO SANA, ISHU IKO HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply