Habari za Michezo
Habari za michezo

ALIYMBEBA MAYELE ATAKIWA HUKU

Staff Desk September 28, 2023 10:34 am

Kocha wa Klabu ya Pyramids ya Misri anayoichezea Fiston Mayele, Mreno Jaime Pacheco ameripotiwa kutakwa na klabu ya Marseille ya Ufaransa ambayo kwa sasa haina kocha mkuu baada ya kuachana na aliyekuwa kocha wao Mhispania Marcelino Garcia Toral ambaye alijiuzulu nafasi hiyo kwa sababu binafsi.

Jamie Pacheco alijiunga na Pyramids FC Januari 2023,na kuiwezesha timu hiyo kumaliza wapili kwenye ligi kuu ya Misri na kupata nafasi ya kushiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika.

Ripoti kutoka nyumbani kwa Jaime Pacheco nchini Ureno zinaeleza kuwa jina la kocha huyo limependekezwa kwa Rais wa Klabu ya Marseille Pablo Longoria ambaye anataraji kufanya maamuzi siku chache zijazo.

HILI NI LETU! MBRAZILI AITISHA KIKAO NA MASTAA UJIO WA AFCON SIMBA YAHUSISHWA…. ISHU IKO HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply