Habari za Simba
Habari za michezo

SIMBA WAIFANANISHA AL AHLY NA ZAMALEK

Staff Desk October 24, 2023 1:45 pm

Uongozi wa Klabu ya Simba imesema kuwa unatambua mchezo wao wa nusu fainali ya African Football League dhidi ya Al Ahly ni mgumu ndani na nje ya uwanja hivyo wamejidhatititi kuhakikisha wanapata matokeo chanya na kusonga mbele.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally wakati akizungumza na wanahabari nchini humo kuelekea mchezo huo utakaopigwa leo Oktoba 24, 2023 nchini Misri baada ya ule wa kwanza kumalizika kwa sare ya bao 2-2 katika Dimba la Mkapa.

“Tunakwenda kucheza kwenye moja ya viwanja vikubwa barani Afrika na wenye heshima kubwa. Uwanja wa Cairo International ni moja ya viwanja vigumu kuvicheza, ndiyo uwanja wa nyumbani wa Al Ahly na Zamalek na ndiyo uwanja wa Taifa wa Misri. Ahly wameuzoea kwa sababu wanautumia kila siku.

“Ni mechi ngumu lakini Simba tunahitaji kuandika historia mpya baada ya miaka 20 ambapo tulimtoa Zamalek mwaka 2003 kwenye mashindano. Hivyo tunataka kuwatoa wapinzani wa Zamalek katika uwanja huo huo.

“Tunajua ugumu wa mechi kuanzia nje mpaka ndani ya uwanja, mashabiki wao watajaa, watashangilia, wataimba mwanzo mwisho kwa nguvu, lakini sisi tutapambana na vikwazo vyote vya ndani na nje ya uwanja ili wachezaji wetu wajikitike kwenye mechi uwanjani tu,” amesema Ahmed.

WAKATI LEO NI ROUND YA PILI YA AFL…SIMBA WAFUNIKA TIMU ZOTE KWA TAKWIMU…. SIMBA KUVUNA MKWANJA HUU WAKIMTOA AL AHLY LEO….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply