Habari za Michezo
Habari za michezo

GAMONDI AIPIGA CHABO SIMBA KWA MKAPA….

admin October 28, 2023 9:05 pm

Kocha Mkuu wa Yanga, Miguel Gamondi na Meneja wa timu hiyo Walter Haryson wametinga katika Uwanja wa Mkapa kutazama mchezo wa Ligi kuu Bara kati ya Simba dhidi ya Ihefu.

Gamondi ameingia mapema kwenye uwanja nusu saa kabla ya mchezo huo kuanza na kushuhudia wachezaji wa timu hizo wakipasha misuli joto.

Gamondi amefika uwanjani kwa ajili ya kuwatazama wapinzani wao Simba ambao watakutana mchezo unaofuata Novemba 5 mwaka huu katika uwanja huo huo.

Kocha huyo amekuwa na utaratibu wa kwenda kutazama mechi wapinzani wao Simba kwani hata kwenye mchezo wa African Football League dhidi ya Al Ahly alikuwepo uwanjani.

MANARA:- SIMBA WAMEIHESHIMISHA NCHI…ZAMANI HAIKUWA HIVI KABISA… MAXI, PACOME WAPEWA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply