Home Habari za michezo AZIZ KI ATHIBITISHA KUWA YEYE NI MASTER

AZIZ KI ATHIBITISHA KUWA YEYE NI MASTER

FT: YANGA 3-2 AZAM FC

Wakati Yanga wakiendelea kushangilia ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya waoka Mikate wa Azam FC.

Kuna mtu mmoja kutoka Taifa la Burkinafaso aliliona hilo akaamua kujivika jukumu la ushujaa kwa upande wa Wannachi.

Wakati ufanyaji wa maamuzi na pasi sahihi kwenye maeneo ya mbele yalionekana kutokuwa sahihi kutoka kwa timu zote mbili pengine kutokana na presha ya mchezo na ndio maana uwezo binafsi umeonekana kutokea pande zote mbili lakini kama unahitaji uwezo binafsi wa mtu mmoja tu ukuamulie mechi ya mpira wa miguu basi utaupata kwa Stephane Aziz Ki.

Ball Striking ya Aziz Ki ikiwa kwenye full flow inakufanya uone kuwa ukilenga goli tu basi umefunga lakini ukweli ni kwamba it’s far from that. Jamaa anajua kupiga haswa na anazijua angle zake vizuri.

SOMA NA HII  BAADA YA KUWATAZAMA AL AHLY JUZI....GAMONDI KATABASAMU KISHA AKASEMA HAYA...