Chama na Simba SC Msimu Huu
Habari za michezo

KWA HILI LA CHAMA NI WAZI MAMBO SIO MAMBO MSIMU HUU

Staff Desk November 10, 2023 12:29 am

Mwamba wa Lusaka, Clatous Chama mkali wa pasi za mwisho Novemba 8 2023 anatimiza saa 792 za kuganda bila kushangilia pasi yake ya bao wala kufunga ndani ya Ligi Kuu Bara.

Ikumbukwe kwamba Oktoba 5 2023 ilikuwa ni mara ya mwisho kwa staa huyo wa Simba raia wa Zambia kufunga ndani ya ligi kwa msimu wa 2023/24.

Alifunga bao hilo kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Tanzania Prisons uliochezwa Uwanja wa Sokoine Mbeya walipokomba pointi tatu ugenini.

Baada ya dakika 90 ubao ulisoma Tanzania Prisons 1-3 Simba. Kwenye mechi zilizofuata mwamba huyo aliganda kwa kushindwa kufunga wala kutoa pasi ya bao.

Siku 33 zimeyeyuka kwa staa huyo kushindwa kuonyesha makali yake kwenye kikosi hicho. Alikuwa shuhuda ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Simba 1-5 Yanga katika Kariakoo Dabi iliyochezwa Novemba 5.

Msimu wa 2022/23 Chama alikuwa ni namba moja kwenye kutoa pasi za mwisho alipotoa pasi 14 za mabao upepo umekuwa mgumu msimu huu akiwa katoa pasi moja ya bao na kutupia mabao mawili.

SIMBA HALI SI SHWARI LIGI KUU…… NAMUNGO WAFANYA UKATILI WA KULAZIMISHANA MAXI AWAPA WACHEZAJI WA YANGA KAULI HII YA KISHUJAA KUHUSU KIPIGO CHA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply