Habari za michezo

AHMED ALLY AWATULIZA MASHABIKI WA SIMBA

Staff Desk November 26, 2023 12:27 pm

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, timu ya Simba SC, imebanwa mbavu nyumbani kwa kulazimishwa sare ya 1-1 na Asec Mimosa ya Ivory Coast.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo kumalizika, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amewatuliza mashabiki wa timu hiyo akisema kuwa kazi bado haijaisha.

“Tumepata alama moja, si nzuri sana na si mbaya sana, Tuna kazi kubwa ya kufanya katika mechi zijazo kuhakikisha malengo yanatimia.

“Bado tuna nafasi ya kufanya vizuri, tumepoteza alama tatu katika 18 za hatua ya makundi hivyo tumebakiwa na 15 za kupigania.

“Nyakati ngumu zinatukomaza na kutukumbusha tuboreshe wapi kwenye timu yetu. Poleni sana Wana Lunyasi.

Msimamo
Galaxy – goli 1, pointi 3, nafasi ya 1
Asec Mimosas – goli 1, pointi 1, nafasi ya 2
Simba Sc – goli 1, pointi 1, nafasi ya 3
Wydad goli 0, pointi 0, nafasi ya 4.

Mechi zijazo
Galaxy vs Simba
Asec vs Wydad

Tangu msimu huu umeanza, Simba haijashinda mchezo wowote wa Kimataifa.

Power Dynamo 2-2 Simba SC
Simba SC 1-1 Power Dynamo
Simba SC 2-2 Al Ahly
Al Ahly 1-1 Simba SC
Simba SC 1-1 Asec Mimosac.

WACHEZAJI SIMBA HALI TETE KIGOGO WA SIMBA AFUNGUKA HAYA HAWA SIMBA, YANGA MBONA KAMA WANATULETEA UTANI KIMATAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply