Benchikha
Habari za michezo

BENCHIKHA ATOA KAULI HII KWA MASHABIKI WA SIMBA

Staff Desk November 28, 2023 1:10 pm

Kocha mpya wa Simba SC, Abdelhak Benchikha ametoa kauli nzito na ya kuwapa faraja mashabiki wa klabu hiyo ambao walikuwa wameikatia tamaa timu yao.

Kupitia kwa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema kocha ametoa kauli hiyo iliyobebwa na maneno mawili tu; mafanikio na ushindi.

“Kocha amezungumza winning and success yaani anaahidi ushindi na mafanikio,” alisema Ahmed Ally.

Kocha huyo raia wa Algeria, ameshaanza kazi Msimbazi ambapo kwa taarifa ya awali, leo atakwenda kuona mazoezi na kesho atakuwa na kikao na mazungumzo na mchezaji mmojammoja.

Kama masuala ya vibali yatakwenda vizuri basi kuna uwezekano mkubwa, wikiendi hii akawa mzigoni Simba itakapoenda ugenini kuvaana na Jwaneng Galaxy nchini Botswana Jumamosi Desemba 2,2023.

UONGOZI SIMBA WAFUNGUKA KILICHOMLETA BENCHIKHA SIMBA GAMONDI NAE HAPOI UNAAMBIWA KABADILI GIA JUU KWA JUU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply