Habari za Simba
Habari za michezo

HATMA YA SIMBA IPO KWA MKAPA UONGOZI WAFUNGUKA HAYA KUHUSU WYDAD

Staff Desk December 11, 2023 12:33 pm

Klabu ya Simba imesema kuwa hatima yao ya kufuzu hatua ya makundi na kwenda robo fainali ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika iko mikononi mwao, Desemba 19, 2023 watakapokutana na mpinzani wao, Wydad Casablanca.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally baada ya kumalizika kwa mchezo wa kwanza uliopigwa Marrakech nchini Misri juzi Jumamosi na Simba kukubali kichapo cha bao 1-0 dakika za lala salama.

“Kwenye kilele cha ubora wetu, tumepoteza mchezo. Kazi nzuri wachezaji wetu mmepambana na kuvuja jasho kwa ajili ya timu yetu lakini dakika za nyongeza zimekua katili kwetu.

“Hatma yetu ipo mikononi mwetu Desemba 19, tunamkaribisha Wydad kwenye Tanuri la Moto Benjamin Mkapa, tutakachomfanya tunajua sisi,” amesema Ahmedy Ally.

1. ASEC Mimosas – pointi 7

2. Jwaneng Galax – pointi 4

3. Wydad Casablanca – pointi 3

4. Simba SC – pointi 2.

HUWEZI KUAMINI, ILA UKWELI WOTE HUU HAPA DADIKA 630 BILA USHINDI SIMBA SC KAZE MAMBO MENGINE YANUKIA IHEFU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply