Habari za michezo

FEI TOTO ATOA NENO HILI BAADA YA SEKHAN KUTUA JANGWANI

Staff Desk December 18, 2023 1:34 pm

Kiungo wa zamani wa Yanga anayekipiga Azam FC kwa sasa, Feisal Salum ‘Fei Toto’ amekiri kiungo mpya aliyetua kwenye timu hiyo, Shekhan Ibrahim Khamis ni bonge la mchezaji mwenye kipaji na uwezo mkubwa, lakini akamuonya mapema kwa kumtaka ajipange kwelikweli kwa vile ametua katika timu yenye presha kubwa.

“Shekhan ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa na ana kipaji namuona mbali, natarajia atafanya vizuri akipewa nafasi na atapata mafanikio makubwa ndani yake,” alisema Fei Toto na kuongeza;

“Najua amekuja timu kubwa, anatakiwa kupambana na kuonyesha kile alichonacho bila kujali anaenda kupambana na mastaa gani. Ni mchezaji ambaye nimemshuhudia ni mdogo wangu ameanza kujulikana sasa, lakini ni mchezaji ambaye amekuzwa na kufanywa bora chini ya JKU amepita kwenye misingi ya soka hivyo naamini atakuwa bora.”

CHAMA KWISHA MANENO HANA JAMBO SIMBA DAKIKA ZAKE NI HIZI TU MAMBO HADHARANI ISHU YA YANGA KUFANYA KIINGILIO BURE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply