Habari za Yanga SC
Habari za michezo

MAMBO HADHARANI ISHU YA YANGA KUFANYA KIINGILIO BURE

Staff Desk December 18, 2023 1:38 pm

Mchambuzi wa masuala ya soka nchini kutoka EA Radio, Ibra Kasuga amefunguka kuhusu Klabu ya Yanga kuamua mashabiki zake waingie bure kwenye mchezo wao wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Medeama FC.

Katika mchezo huo utakaopigwa Jumatano, Desemba 20, 2023 katika Dimba la Mkapa, mfadhili wa Yanga, Ghalib Said Mohammed amenunua tiketi zote za jukwaa la mzunguko, hivyo mashabiki wataingia bure.

“Mechi dhidi ya Medeama sio mechi ya kwanza kwenye hatua ya makundi kwa Yanga, kwa mechi za nyumbani hii ni mechi ya pili, kwa hiyo inategemea mechi iliyopita wameona nini.

“Mechi iliyopita ilikuwa na kiingilio inawezekana waliona hadi dakika ya mwisho kuna kusuasua basi safari hii wamenunua, lakini pia wanaangalia trend ya mashabiki kuingia uwanjani.

“Tangu msimu huu umeanza kwenye Tamasha la Yanga Day wanaangalia je namba ya watu inakuwa kubwa au inakuwa ndogo? kama ni kubwa vizuri ila kama ni ndogo hatutaki picha yenye mapengo. Mwisho wa siku lazima uingie mfukoni,“ amesema Ibra.

FEI TOTO ATOA NENO HILI BAADA YA SEKHAN KUTUA JANGWANI YANGA IWE JUA IWE MVUA MPAKA KIELEWEKE NA STRAIKA HUYU WA ASEC

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply